Iran yathibitisha kuishambulia Israel kwa makombora
HABARI
Published on 02/10/2024

Televisheni ya taifa ya Iran imeangazia taarifa kutoka kwa IRGC (lslamic Revolution Guard Corps) ikithibitisha kuwa "makumi" ya makombora yamerushwa kuelekea Israel, na kutishia shambulio jingine iwapo Israel itajibu.

Iran inasema shambulio hilo la makombora ni la kulipiza kisasi mauaji ya mwezi Julai ya kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh, pamoja na kiongozi wa Hezbollah, Hassan Nasrallah, siku ya Ijumaa - na kwa mauaji ya watu wa Lebanon na Wapalestina.

Inasema jeshi lake la anga lilikuwa limeazimia kulenga "kambi muhimu" na litatangaza maelezo baadaye.

Comments
Comment sent successfully!