Watu 37 wauawa katika shambulio Somalia - Polisi
HABARI
Published on 04/08/2024
Takriban watu 37 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga na watu wenye silaha kulenga eneo maarufu la ufukweni katika mji mkuu wa Somalia, msemaji wa polisi alisema Jumamosi.
Abdifatah Adan Hassan alisema karibu watu 247 walijeruhiwa, baadhi yao vibaya sana.
Picha za video zilionyesha miili kadhaa na watu waliojeruhiwa katika wilaya ya Abdiaziz mjini Mogadishu.
Vyombo vya habari vya ndani vinasema shambulio hilo lilitekelezwa na wanamgambo wa al-Shabab wanaodhibiti sehemu kubwa za kusini na katikati mwa Somalia.
Comments
Comment sent successfully!